Pape Abdoulaye N'daw
Simba iliachana na mipango ya kumchukua Papa Niang baada ya dakika
45 za mechi ya kirafiki katikati ya wiki, ilipogundua kuwa ni 'bomu'.
N'daw naye atakuwa na mtihani rasmi wa kwanza Simba wakati mabingwa
wa Bara wa zamani hao watakapocheza kirafiki dhidi ya Mafunzo kwenye
uwanja Uwanja wa Amaan.
Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba SC, Zacharia Hans Poppe
amesema N’daw aliyetokea klabu ya Dinamo Bucuresti ya Ligi Kuu ya
Romania atacheza pia mechi nyingine Jumapili dhidi ya JKU.
“Baada ya mechi hizo mbili, naamini benchi la ufundi litakuwa
limeona uwezo wake na kuamua kama asajiliwe au aachwe aende," alisema
Hans Poppe na kuahidi "tutasubiri kauli ya kocha wetu juu ya uwezo
wake.”
Aidha, Hans Pope alisema mchezaji kutoka Mali, Makan Dembele ataungana na Simba Zanzibar pindi atakapofika.
“Kumekuwa na vikwazo katika safari yake, lakini tunadhani leo
(jana) atafika na akifika tutampeleka Zanzibar kuungana na wachezaji
wengine ambapo pia Kocha Kerr atatoa maamuzi yake baada ya kumuangalia
uwanjani.
Benchi la ufundi la timu hiyo liliachana na Niang baada ya
kumjaribu kwenye mchezo wa kirafiki dhidi ya Mwadui kwenye Uwanja wa
Taifa Jumatatu.
Kocha wa Simba, Kerr amewaagiza viongozi kumtafutia mshambuliaji
mwenye uwezo juu baada ya kuona waliopo wanashindwa kuzitumia vizuri
nafasi za kufunga zinazopatikana.
CHANZO:
NIPASHE
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni